KATIBA RASMI

EL ELYON CHRISTIAN MINISTRY

"GOD MOST HIGH" - "MUNGU ALIYE JUU ZAIDI"

📍 State of Utah, America 📅 30 Desemba 2022 📋 Namba: 13187391-0140 🔑 Access Code: 6968725
📑 YALIYOMO
  • 1. Jina la Ministry
  • 2. Tafsiri na Utambulisho wa Huduma
  • 3. Msingi wa Kibiblia
  • 4. Tamko la Imani (Statement of Faith)
  • 5. Maono (Vision)
  • 6. Mission / Kusudi la Huduma
  • 7. Malengo ya Ministry
  • 8. Tabia na Nature ya Ministry
  • 9. Makao Makuu na Matawi
  • 10. Eneo la Uendeshaji
  • 11. Uanachama na Ushiriki
  • 12. Makundi ya Washiriki
  • 13. Haki za Washiriki
  • 14. Wajibu wa Washiriki
  • 15. Muundo wa Uongozi
  • 16. Mamlaka ya Kiroho na Kiutendaji
  • 17. Vyeo na Majukumu ya Viongozi
  • 18. Bodi / Baraza la Uongozi
  • 19. Idara za Ministry
  • 20. Mikutano ya Ministry
  • 21. Mfumo wa Maamuzi
  • 22. Maadili ya Huduma
  • 23. Nidhamu na Taratibu za Kinidhamu
  • 24. Utatuzi wa Migogoro
  • 25. Fedha, Mali na Rasilimali
  • 26. Mfumo wa Uhasibu na Uwajibikaji
  • 27. Sadaka, Michango na Mapato
  • 28. Sera ya Ulinzi wa Watoto
  • 29. Sera ya Counseling, Deliverance na Privacy
  • 30. Sera ya Media, Branding na Mawasiliano
  • 31. Sera ya Uinjilisti, Outreach na Misheni
  • 32. Mfumo wa Mafunzo na Ukuaji wa Viongozi
  • 33. Mfumo wa Matawi
  • 34. Mfumo wa Mapitio ya Katiba
  • 35. Kuvunjwa kwa Ministry
  • 36. Uidhinishaji na Sahihi
  • Viambatianisho

📢 Eneo la Uendeshaji wa Huduma:

Mataifa yote kwa mapenzi ya Mungu, ikiwemo Marekani, Tanzania, na nchi zinginezo ambako huduma itapanuliwa kwa utaratibu wa kiroho na kiutawala.

IBARA YA 1: JINA LA MINISTRY

Huduma hii itajulikana rasmi kwa jina la:

EL ELYON CHRISTIAN MINISTRY

Moto: "GOD MOST HIGH"

Msingi: Mwanzo 14:19-20

IBARA YA 2: TAFSIRI NA UTAMBULISHO WA HUDUMA

EL ELYON CHRISTIAN MINISTRY ni huduma ya Kikristo iliyoanzishwa kwa kusudi la:

  • a) Kumtangaza Mungu Aliye Juu Zaidi
  • b) Kumhubiri Yesu Kristo
  • c) Kurejesha watu kwa Mungu
  • d) Kulea waamini katika kweli ya Neno la Mungu
  • e) Kuleta uponyaji, ukombozi, maombi, ibada, na mabadiliko ya kiroho na kijamii

Huduma hii ni ya:

  • a) kiroho
  • b) ya kimaandiko
  • c) ya kinabii kwa msingi wa Biblia
  • d) ya mabadiliko ya maisha

Ikilenga kugusa: roho, nafsi, familia, vijana, wanawake, jamii, na mataifa.

IBARA YA 3: MSINGI WA KIBIBLIA

Huduma hii inasimama juu ya Neno la Mungu na inatambua maandiko yafuatayo:

Zaburi 42:2
2 Wakorintho 6:16
1 Timotheo 4:10
Mathayo 16:16
Waebrania 3:12
Mwanzo 14:19-20
Waebrania 7:1

Maana ya Kiroho ya Msingi

Huduma hii inamtambua Mungu kama:

  • a) Mungu aliye hai
  • b) Mungu anayekaa katikati ya watu wake
  • c) Mungu Mkuu wa mbingu na nchi
  • d) Mungu wa wokovu, rehema, ukombozi, na nguvu

Yesu Kristo

Yesu Kristo ndiye msingi mkuu wa huduma hii, na kila jambo litafanywa kwa msingi wa: Neno la Mungu, Roho Mtakatifu, Kweli, Upendo, Utakatifu, na Utii.

IBARA YA 4: TAMKO LA IMANI (STATEMENT OF FAITH)
  1. EL ELYON CHRISTIAN MINISTRY inaamini kwamba kuna Mungu mmoja wa kweli, aliye hai, wa milele, Muumba wa mbingu na nchi.
  2. Kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu, Bwana na Mwokozi wa ulimwengu.
  3. Kwamba Roho Mtakatifu ni wa Mungu na anatenda kazi ya kuongoza, kufundisha, kutia nguvu, na kuleta mabadiliko kwa waamini.
  4. Kwamba Biblia Takatifu ni Neno la Mungu lenye mamlaka ya mwisho katika mafundisho, maisha, na uendeshaji wa huduma.
  5. Kwamba wokovu hupatikana kwa neema ya Mungu kupitia imani katika Yesu Kristo.
  6. Kwamba maombi, ibada, toba, utakatifu, na maisha ya utii ni sehemu ya msingi ya maisha ya Mkristo.
  7. Kwamba Mungu bado anatenda kazi kwa nguvu zake kupitia: maombi, uponyaji, ukombozi, huduma, uinjilisti, na kujengwa kwa mwili wa Kristo.
  8. Kwamba Kanisa ni mwili wa Kristo na waamini wameitwa kuishi katika upendo, umoja, na huduma.
IBARA YA 5: MAONO (VISION)

"Kuona watu, familia, jamii na mataifa yakimjua Mungu Aliye Juu Zaidi, yakimkiri Yesu Kristo, na kubadilishwa kwa nguvu ya Neno la Mungu na Roho Mtakatifu."

IBARA YA 6: MISSION / KUSUDI LA HUDUMA

"Kumhubiri Kristo, kuombea watu, kuleta ukombozi, kuinua ibada, kulea kizazi cha waamini na viongozi, na kuleta mabadiliko ya kiroho na kijamii kupitia huduma ya Neno, maombi, ibada, media, outreach, na misheni."

IBARA YA 7: MALENGO YA MINISTRY

7.1 Malengo ya Kiroho

  • a) Kuhubiri Injili ya Yesu Kristo
  • b) Kuleta wokovu kwa watu
  • c) Kulea maisha ya maombi
  • d) Kufundisha Neno la Mungu
  • e) Kuleta ukombozi na uponyaji wa kiroho

7.2 Malengo ya Uongozi

  • a) Kuibua na kulea viongozi wa kiroho
  • b) Kuandaa watumishi waaminifu
  • c) Kujenga mfumo wa huduma wenye nidhamu na uwajibikaji

7.3 Malengo ya Jamii

  • a) Kusaidia jamii kwa upendo wa Kristo
  • b) Kuleta mabadiliko chanya kwa vijana, wanawake, familia na watu wenye uhitaji
  • c) Kufanya huduma za kijamii kwa misingi ya imani na utu

7.4 Malengo ya Kimataifa

  • a) Kufungua matawi na vituo vya huduma kwa utaratibu
  • b) Kufanya outreach na missions
  • c) Kutumia media kufikia mataifa
IBARA YA 8: TABIA NA NATURE YA MINISTRY

Huduma hii itakuwa:

  • a) ya Kikristo
  • b) ya kibiblia
  • c) ya maombi
  • d) ya ibada
  • e) ya uinjilisti
  • f) ya ukombozi
  • g) ya kujenga jamii
  • h) ya nidhamu
  • i) ya uwajibikaji
  • j) ya uongozi wa kiroho
  • k) ya huduma ya ndani na ya kimataifa
IBARA YA 9: MAKAO MAKUU NA MATAWI

9.1 Makao Makuu

Salt Lake City, Utah, Marekani (USA)

9.2 Uendeshaji wa Tanzania

Huduma hii itafunguliwa na kuendeshwa pia Tanzania kama eneo rasmi la huduma na upanuzi wa ministry.

9.3 Vitungu vingine

Ofisi, vituo, makanisa, prayer centers, mission points, media offices au matawi yanaweza kufunguliwa katika maeneo mengine kwa idhini ya uongozi mkuu wa ministry.

IBARA YA 10: ENEO LA UENDESHAJI

Huduma hii inaweza kufanya kazi katika:

Marekani
Tanzania
Afrika
Mataifa mengine

Kwa njia zifuatazo:

  • a) mikutano ya ana kwa ana
  • b) ibada
  • c) crusades
  • d) semina
  • e) conferences
  • f) missions
  • g) online ministry
  • h) livestreams
  • i) social media
  • j) media broadcasts
  • k) community programs
IBARA YA 11: UANACHAMA NA USHIRIKI

EL ELYON CHRISTIAN MINISTRY itakuwa na mfumo wa ushiriki unaojumuisha watu binafsi, viongozi, washirika, na watumishi wanaoshiriki huduma kwa imani, maadili, na utaratibu wa ministry.

11.1 Mtu anaweza kuwa sehemu ya ministry hii ikiwa:

  • a) anamkiri Yesu Kristo au yuko katika safari ya kujifunza na kukua kiroho
  • b) anakubaliana na msingi wa ministry
  • c) yuko tayari kuheshimu katiba na maadili ya ministry
  • d) yuko tayari kuwa chini ya utaratibu wa huduma
IBARA YA 12: MAKUNDI YA WASHIRIKI

Kutakuwa na makundi yafuatayo:

12.1 Founding Leadership / Founding Team

Watu waliohusika moja kwa moja katika kuanzishwa na msingi wa huduma.

12.2 Registered Members

Washirikiwaliotambuliwa rasmi ndani ya ministry.

12.3 Active Workers / Volunteers

Watu wanaohudumu katika idara mbalimbali.

12.4 Ministry Partners

Watu au taasisi zinazounga mkono huduma kwa maombi, fedha, vifaa, au huduma nyingine.

12.5 Department Leaders

Viongozi wa idara maalum ndani ya ministry.

12.6 Branch / Regional Leaders

Viongozi wa matawi au vituo vya huduma.

12.7 Advisors / Elders / Spiritual Counsel

Watu wenye nafasi ya ushauri wa kiroho au kitaasisi.

IBARA YA 13: HAKI ZA WASHIRIKI

Kila mshiriki mwenye hadhi rasmi ndani ya ministry atakuwa na haki ya:

  • a) kupokea huduma ya kiroho kwa heshima
  • b) kushiriki ibada, maombi, mafundisho na huduma halali za ministry
  • c) kupata mwongozo wa kiroho kwa utaratibu
  • d) kusikilizwa kwa haki kwenye masuala ya ndani ya ministry
  • e) kushiriki katika shughuli halali za ministry kulingana na nafasi yake
  • f) kulindwa utu wake, faragha yake, na usalama wake
IBARA YA 14: WAJIBU WA WASHIRIKI

Kila mshiriki atawajibika:

  • a) kuishi kwa heshima na maadili ya Kikristo
  • b) kuheshimu viongozi halali wa ministry
  • c) kufuata katiba, maadili, na taratibu za huduma
  • d) kutunza umoja wa mwili wa Kristo
  • e) kutotumia ministry kwa maslahi binafsi
  • f) kutunza siri na heshima ya watu wengine
  • g) kushiriki kwa uaminifu katika huduma aliyopewa
IBARA YA 15: MUUNDO WA UONGOZI

EL ELYON CHRISTIAN MINISTRY itakuwa na muundo wa uongozi unaolinda: maono, kweli ya Neno, uwajibikaji, nidhamu, usalama wa huduma, na uendelevu wa taasisi.

15.1 Ngazi za Uongozi

  • a) Founder / Vision Bearer
  • b) Spiritual Overseer / Senior Leader
  • c) Board of Leadership / Governing Council
  • d) Executive Leadership Team
  • e) Department Leaders
  • f) Branch / Regional Leaders
  • g) Workers / Volunteers
  • h) Members / Partners
IBARA YA 16: MAMLAKA YA KIROHO NA KIUTENDAJI

16.1 Mamlaka ya Kiroho

Hii inahusu: mafundisho, maombi, ibada, ushauri wa kiroho, maono ya huduma, na mwelekeo wa kiroho wa ministry.

16.2 Mamlaka ya Kiutendaji

Hii inahusu: fedha, operations, ratiba, approvals, usimamizi wa watu, vifaa, records, systems, communication, na event management.

16.3 Mipaka ya Mamlaka

Hakuna mtu atakayekuwa na mamlaka yasiyo na mipaka. Kila mamlaka ndani ya ministry lazima yawe: halali, yanayoeleweka, yenye uwajibikaji, na yanayoweza kukaguliwa.

IBARA YA 17: VYEO NA MAJUKUMU YA VIONGOZI

17.1 FOUNDER / VISION BEARER

Majukumu: Kulinda maono na msingi wa huduma, Kutoa mwelekeo mkuu wa kiroho, Kusimamia integrity ya huduma, Kushauri uongozi wa juu, Kuthibitisha mwelekeo wa upanuzi wa huduma.

Mipaka: Hatakuwa juu ya katiba kwa namna ya kuvunja uwajibikaji, Atashauriana na uongozi na bodi katika masuala ya taasisi, fedha, mali na maamuzi makubwa.

17.2 SPIRITUAL OVERSEER / SENIOR LEADER

Majukumu: Kusimamia huduma za kiroho, Kufundisha, kuongoza maombi na ibada, Kusimamia viongozi wa huduma, Kulinda usafi wa mafundisho, Kutoa direction ya kiroho kwa ministry.

17.3 GOVERNING COUNCIL / BOARD OF LEADERSHIP

Kazi: Kusimamia governance ya ministry, Kulinda uwajibikaji, Kusimamia matumizi makubwa ya rasilimali, Kupitia taarifa za fedha, Kupitisha sera kuu, Kusimamia uhalali wa maamuzi makubwa.

Muundo: Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu, Mweka Hazina, Wajumbe, Mshauri wa Kiroho, Mshauri wa Sheria/Usimamizi.

17.4 EXECUTIVE LEADERSHIP TEAM

Hii ni timu ya uendeshaji wa kila siku. Inaweza kujumuisha: Director, Operations Leader, Ministry Coordinator, Admin Officer, Finance Officer, Media Lead, Outreach Lead, Youth/Women Leads, Prayer/Deliverance/Worship Leads.

17.5 KATIBU WA MINISTRY

Majukumu: Kutunza kumbukumbu zote rasmi, Kuandaa agenda na minutes, Kutunza nyaraka za katiba, mikutano, na maamuzi, Kusimamia taarifa za ndani.

17.6 MWEKA HAZINA / FINANCE LEAD

Majukumu: Kusimamia mapato na matumizi, Kutunza records za fedha, Kutoa taarifa za fedha, Kuhakikisha matumizi yote yanafuata taratibu, Kusimamia mfumo wa receipts, approvals, na reporting.

17.7 VIONGOZI WA IDARA

Kila idara itakuwa na kiongozi rasmi atakayewajibika kwa: uratibu wa idara, watu wake, ratiba, discipline, reporting, na utendaji wa huduma.

IBARA YA 18: BODI / BARAZA LA UONGOZI

Kutakuwa na Baraza/Bodi ya Uongozi la ministry litakalokuwa chombo cha juu cha usimamizi wa taasisi kwa upande wa governance na accountability.

18.2 Majukumu ya Bodi

  • a) Kupitia na kupitisha sera kuu
  • b) Kusimamia integrity ya ministry
  • c) Kusimamia matumizi ya rasilimali
  • d) Kupokea na kujadili reports za utendaji
  • e) Kusimamia upanuzi wa ministry
  • f) Kusimamia compliance ya taasisi

18.3 Muda wa huduma

Wajumbe wa bodi wanaweza kuhudumu kwa kipindi kitakachowekwa na ministry, kwa mfano miaka 3, na wanaweza kurejeshwa kwa mujibu wa uhitaji na maamuzi halali ya ministry.

IBARA YA 19: IDARA ZA MINISTRY

EL ELYON CHRISTIAN MINISTRY itakuwa na idara zifuatazo:

19.1 Evangelism Ministry

Kusudi: Kuhubiri Injili ya Yesu Kristo kwa watu binafsi, jamii, maeneo mapya, na mataifa.

Kazi: street evangelism, house-to-house evangelism, crusades, soul winning, missions, discipleship follow-up

19.2 Deliverance Ministry

Kusudi: Kuhudumia watu kwa maombi ya ukombozi, uponyaji wa kiroho, na msaada wa kiimani kwa utaratibu salama na wa kibiblia.

Sharti: Huduma hii lazima ifanywe kwa heshima, privacy, na accountability bila unyanyasaji wa aina yoyote

19.3 Worship Ministry

Kusudi: Kuongoza watu katika ibada ya kweli mbele za Mungu.

Kazi: praise & worship, worship events, choir / worship teams, worship training

19.4 Prayer Ministry

Kusudi: Kusimamia madhabahu ya maombi ya ministry.

Kazi: prayer meetings, intercession, fasting programs, spiritual watch

19.5 Youth Ministry

Kusudi: Kulea na kujenga kizazi cha vijana kwa msingi wa Kristo.

19.6 Women Ministry

Kusudi: Kuinua wanawake katika imani, maombi, maadili, huduma, na mabadiliko ya maisha.

19.7 Media Ministry

Kusudi: Kutumia media kueneza Injili na maono ya ministry.

Kazi: video, audio, livestream, social media, graphics, publications, content production

19.8 Outreach / Missions Ministry

Kusudi: Kufikisha huduma kwa maeneo ya nje na yenye uhitaji wa kiroho au kijamii.

19.9 Community Transformation Ministry

Kusudi: Kugusa jamii kwa upendo wa Kristo kupitia mabadiliko ya kijamii, utu, msaada, elimu, malezi, na uwezeshaji wa msingi.

IBARA YA 20: MIKUTANO YA MINISTRY

20.1 Mikutano rasmi ifuatayo:

  • Mikutano ya Kawaida: ya maombi, ya ibada, ya viongozi, ya idara, ya wafanyakazi/watendaji, ya washirika
  • Mikutano ya Uongozi: Uongozi mkuu utakutana mara kwa mara kwa mujibu wa ratiba ya ministry.
  • Mikutano ya Dharura: Inaweza kuitishwa na kiongozi mkuu au mamlaka husika kwa jambo la haraka.

20.4 Kumbukumbu

Kila mkutano rasmi utakuwa na: agenda, attendance, minutes, na action points.

IBARA YA 21: MFUMO WA MAAMUZI

21.1 Maamuzi

Maamuzi ndani ya ministry yatafanywa kwa: maombi, ushauri wa Neno la Mungu, utaratibu wa uongozi, uwajibikaji, na hekima.

21.2 Maamuzi makubwa

Maamuzi makubwa yatahitaji majadiliano ya uongozi husika, na inapobidi, idhini ya Baraza/Bodi au uongozi mkuu.

21.3 Maamuzi makubwa ni pamoja na:

  • a) kufungua tawi jipya
  • b) kununua/kukodisha mali
  • c) matumizi makubwa ya fedha
  • d) kuanzisha project kubwa
  • e) mabadiliko ya katiba
  • f) uteuzi wa viongozi wa juu
  • g) masuala ya nidhamu ya viongozi wa juu
IBARA YA 22: MAADILI YA HUDUMA

Kila mshiriki, mtumishi, kiongozi au mwakilishi wa ministry anatakiwa kuishi kwa: utakatifu, uaminifu, heshima, unyenyekevu, ukweli, kujizuia, upendo, uwajibikaji, na heshima ya mwili wa Kristo.

22.1 Hairuhusiwi:

  • a) kutumia ministry kwa faida binafsi kwa njia isiyo halali
  • b) unyanyasaji wa aina yoyote
  • c) lugha ya matusi au fedheha
  • d) ubaguzi usio wa kibiblia
  • e) matumizi mabaya ya fedha
  • f) matumizi mabaya ya mamlaka ya kiroho
  • g) kutumia madhabahu/platform vibaya
  • h) kushusha hadhi ya watu au kuwatawala kwa hofu ya kiroho
IBARA YA 23: NIDHAMU NA TARATIBU ZA KINIDHAMU

Kila mshiriki wa ministry atawajibika kinidhamu ikiwa atakiuka katiba, maadili, taratibu, au uaminifu wa huduma.

23.2 Hatua za kinidhamu zinaweza kujumuisha:

  • a) onyo la mdomo
  • b) onyo la maandishi
  • c) kusimamishwa kwa muda
  • d) kuondolewa kwenye huduma fulani
  • e) kuondolewa kwenye nafasi ya uongozi
  • f) kufutwa ushiriki wa ndani wa ministry kwa mujibu wa uzito wa jambo

Hakuna hatua ya kinidhamu itakayochukuliwa kwa upendeleo au chuki; haki, ushahidi, ushauri, na utaratibu vitazingatiwa.

IBARA YA 24: UTATUZI WA MIGOGORO

Migogoro ya ndani ya ministry itashughulikiwa kwa: maombi, ushauri, usuluhishi, ushuhuda wa kweli, na utaratibu wa kiroho na kiutawala.

24.2 Migogoro inaweza kuwa ya:

  • a) viongozi
  • b) washiriki
  • c) idara
  • d) fedha
  • e) maadili
  • f) huduma
  • g) matumizi ya mamlaka

Migogoro yote itapelekwa kwa ngazi husika ya uongozi, na inapobidi kwa Baraza/Bodi ya Uongozi.

IBARA YA 25: FEDHA, MALI NA RASILIMALI

25.1 Mapato ya ministry yanaweza kutoka kwa:

  • a) sadaka
  • b) michango
  • c) donations
  • d) partnerships
  • e) support offerings
  • f) fundraising
  • g) sponsorships
  • h) projects halali
  • i) media support
  • j) gifts halali za huduma

25.2 Mali ya ministry inaweza kujumuisha:

  • a) fedha
  • b) vifaa
  • c) instruments
  • d) media equipment
  • e) samani
  • f) magari
  • g) ardhi
  • h) majengo
  • i) rights za media na publications
  • j) accounts za ministry
  • k) branding assets

Mali yote ya ministry ni ya ministry, si ya mtu binafsi.

IBARA YA 26: MFUMO WA UHASIBU NA UWAJIBIKAJI

Fedha zote za ministry zitahifadhiwa na kusimamiwa kwa mfumo wa uwajibikaji.

26.2 Kutakuwa na:

  • a) records za mapato
  • b) records za matumizi
  • c) receipts
  • d) approvals
  • e) reporting
  • f) reconciliation
  • g) accountability system

26.4 Kutakuwa na utaratibu wa:

  • a) signer approvals
  • b) petty cash control
  • c) procurement control
  • d) donation recording
  • e) asset register
  • f) financial reporting

Taarifa za fedha zitatolewa kwa uongozi kwa vipindi maalum.

IBARA YA 27: SADAKA, MICHANGO NA MAPATO

Sadaka, michango, au msaada wowote utapokelewa kwa heshima, uwazi, na uadilifu.

Hakna mtu atakayelazimishwa kutoa kwa njia ya udhalilishaji, shinikizo la kisaikolojia, au matumizi mabaya ya mamlaka ya kiroho.

27.3 Matumizi ya fedha yatakuwa kwa:

  • a) huduma
  • b) maendeleo ya ministry
  • c) outreach
  • d) support activities
  • e) administration halali
  • f) projects za huduma
IBARA YA 28: SERA YA ULINZI WA WATOTO NA WATU WENYE UHITAJI WA ULINZI

Ministry itawajibika kulinda watoto, vijana wadogo, wanawake walio kwenye mazingira magumu, na watu wote walio katika mazingira ya uhitaji wa ulinzi.

28.2 Sharti

Hakuna huduma kwa watoto au watu walio hatarini itakayofanyika bila: utaratibu wa usalama, heshima, accountability, na mipaka salama ya huduma.

28.3 Hairuhusiwi:

  • a) unyanyasaji wa aina yoyote
  • b) mgusano usiofaa
  • c) matumizi mabaya ya mamlaka
  • d) mazungumzo au mazingira yasiyo salama
IBARA YA 29: SERA YA COUNSELING, DELIVERANCE NA PRIVACY

Huduma ya ushauri, maombezi, deliverance, na msaada wa kiroho itafanywa kwa heshima, hekima, na faragha.

Taarifa binafsi za watu hazitafichuliwa hovyo bila sababu halali ya huduma au usalama.

29.3 Hairuhusiwi:

  • a) kutumia siri za watu kuwatawala
  • b) kutumia "neno la kiroho" kum-control mtu
  • c) kufanya huduma za faragha kwa mazingira hatarishi yasiyo na accountability
  • d) matumizi mabaya ya mgusano wa mwili
IBARA YA 30: SERA YA MEDIA, BRANDING NA MAWASILIANO

EL ELYON CHRISTIAN MINISTRY itakuwa na utambulisho rasmi wa media na mawasiliano.

Media zote rasmi za ministry zitadhibitiwa na mamlaka halali ya ministry.

Hakuna mtu atakayetoa tangazo rasmi, statement rasmi, au content rasmi kwa niaba ya ministry bila ruhusa halali.

30.4 Matumizi ya:

  • a) logo
  • b) jina la ministry
  • c) kurasa za social media
  • d) livestreams
  • e) videos
  • f) testimonies
  • g) recordings

yatafanyika kwa nidhamu, uhalali, na heshima.

IBARA YA 31: SERA YA UINJILISTI, OUTREACH NA MISHENI

Huduma zote za uinjilisti, outreach, na missions zitafanywa kwa: upendo, heshima, hekima, utii wa Neno la Mungu, na usalama wa washiriki.

Hakna outreach au mission ya ministry itakayofanyika bila uratibu wa viongozi husika.

31.3 Shughuli zote za field zitakuwa na:

  • a) ratiba
  • b) team leadership
  • c) safety coordination
  • d) accountability ya vifaa na fedha
  • e) report ya baada ya huduma
IBARA YA 32: MFUMO WA MAFUNZO NA UKUAJI WA VIONGOZI

Ministry itawekeza katika: mafunzo ya kiroho, mafunzo ya huduma, malezi ya tabia, uongozi, accountability, na practical ministry skills.

32.2 Masharti

Hakna mtu atakayepandishwa katika huduma ya uongozi kwa msingi wa kipawa pekee bila kuangaliwa: tabia, uaminifu, utayari wa kuhudumu, uwajibikaji, na maturity ya kiroho.

32.3 Mfumo wa Ualelewaji

Viongozi watalelewa kwa mfumo wa: mentorship, observation, assignment, accountability, na review.

IBARA YA 33: MFUMO WA MATAWI YA TANZANIA NA NCHI NYINGINE

EL ELYON CHRISTIAN MINISTRY inaweza kufungua matawi, prayer centers, mission centers, worship centers, au offices katika Tanzania na mataifa mengine.

33.2 Masharti ya Tawi

Tawi lolote litakalofunguliwa lazima:

  • a) litambue katiba hii
  • b) litii uongozi mkuu
  • c) liheshimu statement of faith ya ministry
  • d) litumie systems halali za uwajibikaji

Tawi lolote halitakuwa na mamlaka ya kujitenga, kubadili jina, au kutumia mali za ministry nje ya utaratibu wa ministry kuu.

33.5 Tanzania

Kwa upande wa Tanzania, ministry itaheshimu pia taratibu na mahitaji ya kisheria ya eneo husika pale inapohitajika kwa uendeshaji wa ndani wa taasisi au tawi.

IBARA YA 34: MFUMO WA MAPITIO YA KATIBA

Katiba hii inaweza kufanyiwa marekebisho pale inapohitajika kwa ajili ya: ukuaji wa huduma, uwazi zaidi, ufanisi, mabadiliko ya kiutendaji, na upanuzi wa ministry.

34.2 Masharti ya Marekebisho

Marekebisho yoyote lazima: yapendekezwe kwa utaratibu, yajadiliane na uongozi husika, na yapitishwe kwa mamlaka halali ya ministry.

Hakna marekebisho yatakayofanywa kwa namna inayoharibu msingi wa kiimani, maono, au integrity ya huduma bila mchakato rasmi.

IBARA YA 35: KUVUNJWA KWA MINISTRY (DISSOLUTION CLAUSE)

Ikiwa kwa sababu yoyote ministry itasitishwa au kuvunjwa kwa utaratibu halali:

  • a) mali zake hazitagawanywa kama mali binafsi
  • b) rasilimali zake zitatumika kwa kusudi halali la huduma, imani, au taasisi yenye kusudi linalofanana kwa mujibu wa maamuzi ya mamlaka halali ya ministry

Kumbukumbu, mali, na fedha zitasimamiwa kwa uwajibikaji hadi mchakato wa mwisho ukamilike.

IBARA YA 36: UIDHINISHAJI NA SAHIHI

Katiba hii imeandaliwa na kupitishwa kuwa msingi rasmi wa uendeshaji wa:

EL ELYON CHRISTIAN MINISTRY

"GOD MOST HIGH"

ikiwa ni hati ya kuongoza: maono, mafundisho, uongozi, nidhamu, uwajibikaji, huduma, matawi, fedha, na maendeleo ya ministry kwa utukufu wa Mungu.

IMEIDHINISHWA NA:





VIAMBATANISHO VYA MUHIMU

APPENDIX A — CODE OF CONDUCT

Hii ni document ya ndani ya viongozi na watumishi kuhusu: tabia, mavazi, communication, purity, confidentiality, matumizi ya platform, social media conduct, respect and boundaries.

APPENDIX B — FINANCIAL POLICY

Hii iweke: nani anakusanya sadaka, nani anahesabu, nani anaweka benki, approvals za matumizi, petty cash limits, reporting ya mwezi, signatories, procurement controls.

APPENDIX C — SAFEGUARDING POLICY

Hii ni muhimu kwa: watoto, youth, women, vulnerable people, counseling, deliverance.

APPENDIX D — MEDIA POLICY

Hii iweke: access ya social media, approvals za posting, logo usage, photo/video permissions, handling ya testimonies, livestream protocols.

APPENDIX E — TANZANIA BRANCH GOVERNANCE POLICY

Hii ni ya branch ya Tanzania, iweke: local leadership, branch reporting, local finance, branch registration/compliance support, relation na HQ USA.

APPENDIX F — DEPARTMENTAL MANUALS

Kila department iwe na mini-manual yake: Evangelism, Deliverance, Worship, Prayer, Youth, Women, Media, Outreach/Missions, Community Transformation.